top of page
Makala za Mwanadikala


ATCL na Ndoto ya Ndege Nane Mpya: Uwekezaji wa Kimkakati au Kuendelea Kufadhili Hasara?
Na. Rev. Godwin Chilewa Nianze kwa kuweka angalizo kwamba makala hii haijadili kama Tanzania inahitaji shirika la Ndege, bali kama njia inayotumika kuliendesha ina mantiki kiuchumi? Kwa maana uhitaji wa shirika la ndege ni suala moja na mchakato wa kuliendesha ni suala lingine. Uamuzi wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kuongeza ndege nane ifikapo mwaka 2030 umeibua mjadala mpana kuhusu uhalali wa kuendelea kuwekeza fedha nyingi za umma katika sekta ya anga wakati shirika
6 hours ago


KESI YA TUNDU LISSU: Siasa, Usalama, na Mustakabali wa Tanzania
Na Rev. Godwin Chilewa Katika historia ya siasa za Tanzania, kumekuwa na nyakati chache sana ambazo kesi ya mtu mmoja imebeba uzito mkubwa kiasi cha kuathiri mwelekeo mzima wa taifa. Kesi ya Tundu Lissu ni mojawapo ya nyakati hizo. Kesi hii ni ya kipekee kisheria, na ni kioo kinachoakisi mvutano wa ndani wa mfumo wa kisiasa wa Tanzania kati ya udhibiti wa dola na wito wa mageuzi ya kidemokrasia. Tundu Lissu ni mwanasiasa wa aina yake katika uwanja wa siasa za Tanzania. Kwa z
8 hours ago


TISS Isifanye Kosa Lililofanywa na CIA
Katika ulimwengu wa intelijensia, makosa makubwa hayaanzi na kutopatikana kwa taarifa bali kwa namna taarifa hizo zinavyotafsiriwa. Hivyo miongoni mwa makosa hatari zaidi ya kiitelijensia ni kile kinachoitwa confirmation bias. Hili ni tatizo la kisaikolojia linaloweza kuyumbisha maamuzi ya kitaifa na hata kusababisha majanga ya kisiasa, umwagaji damu, na migogoro ya kidiplomasia. Confirmation bias ni hali ambapo mchambuzi wa idara ya usalama au taasisi huchagua, kuamini, au k
5 days ago


URITHI WA MADARAKA AU DEMOKRASIA?
Na Rev. Godwin Chilewa Kifo cha ghafla cha Seneta mashuhuri wa Marekani, Lindsey Graham, kimeacha gumzo kubwa kisiasa kwa sababu ya pengo la uongozi wake, Hata hivyo hatua ya dada yake, Darline Graham Nordone, kuchukua nafasi yake katika Seneti imewaacha hoi hata wale waliozoea kupora madaraka! Wengi wanajiuliza kama huu ni urithi wa kisiasa? Au ni utekelezaji halali wa sheria? na kama ni utaratibu wa kisheria nini athari zake kwa mustakabali wa demokrasia, hasa kwa nchi za
Jul 16


Siasa za Vita na Uadui Zitajenga Taifa?
Na Rev. Godwin Chilewa Katika katiba ya Jamhuri ya Muungano na sera, Tanzania ni taifa linalofuata mfumo wa vyama vingi. Lakini katika uhalisia wa kisiasa, mienendo yake mara nyingi hutoa taswira ya mfumo wa chama kimoja uliovaa vazi jipya. Tofauti kati ya nadharia na vitendo inajionesha bayana katika siasa za nchi, huku ushindani unaotarajiwa kuzaa hoja mbadala na uwajibikaji umegeuka kuwa uadui unaoziba milango ya mazungumzo ya kitaifa. Hiyo ndiyo Tanzania. Mizizi ya tatizo
Jul 15


Georgia Guidestones: Jiwe la Siri, Ajenda ya Dunia, au Tafsiri Iliyopotoshwa?
Je, umewahi kusikia habari za Georgia Guidestones, mnara wa mawe uliosimama kwa miongo kadhaa katika jimbo la Georgia, nchini Marekani? Wengi wa walioujua waliuita “Stonehenge ya Marekani,” wakiufananisha na ule mnara wa kale wa mawe uliopo nchini Uingereza. Lakini kwa wengine ulikuwa zaidi ya sanaa, ulikuwa ujumbe wa siri, ajenda ya dunia mpya, na mwongozo wa kizazi kijacho baada ya maangamizi. Mnara huu ulijengwa mwaka 1980 katika eneo la Elbert County. Jambo lililozua u
Jul 13


Tanzania Kwenye Mizani ya Jumuia ya Madola na Aibu ya Kidiplomasia
Rev. Godwin Chilewa Tamko la Commonwealth Ministerial Action Group (CMAG) la tarehe 10 Julai 2026 ni waraka mzito wenye lugha ya tahadhari, ishara za adhabu zinazotunyemelea, na ujumbe wa wazi kwamba Tanzania imeanza kupoteza uaminifu katika misingi ya utawala bora, haki za binadamu, na demokrasia, misingi ambayo ni uti wa mgongo wa Jumuiya ya Madola. Baada ya matukio ya umwagaji damu tarehe 29 Oktoba 2025, tamko hili halipaswi kusomwa kama maneno ya kawaida ya “diplomasia l
Jul 11


Je, Serikali ya Tanzania Inalea Makundi ya Kigaidi?
Na. Rev. Godwin Chilewa Kauli ya Shekhe Mwaipopo kwamba ana makundi mawili ya vijana, Mbwa Mwitu na Tiger waliopatiwa mafunzo ya kijeshi, na kwamba watatumika kuwaangamiza vijana watakaoandamana tarehe 7 Julai si kauli ya mzaha. Ni kauli nzito, ya kutisha, na yenye harufu kali ya ugaidi. Ikiwa vyombo vya ulinzi na usalama vitakaa kimya na bila kumkamata shekhe huyo na majeshi yake, basi dunia itachukulia ukimya huo kama hatua ya kuhalalisha vurugu, umwagaji damu, na hofu kama
Jul 5
bottom of page


