top of page
Makala za Mwanadikala


Siasa za Vita na Uadui Zitajenga Taifa?
Na Rev. Godwin Chilewa Katika katiba ya Jamhuri ya Muungano na sera, Tanzania ni taifa linalofuata mfumo wa vyama vingi. Lakini katika uhalisia wa kisiasa, mienendo yake mara nyingi hutoa taswira ya mfumo wa chama kimoja uliovaa vazi jipya. Tofauti kati ya nadharia na vitendo inajionesha bayana katika siasa za nchi, huku ushindani unaotarajiwa kuzaa hoja mbadala na uwajibikaji umegeuka kuwa uadui unaoziba milango ya mazungumzo ya kitaifa. Hiyo ndiyo Tanzania. Mizizi ya tatizo
15 hours ago


Georgia Guidestones: Jiwe la Siri, Ajenda ya Dunia, au Tafsiri Iliyopotoshwa?
Je, umewahi kusikia habari za Georgia Guidestones, mnara wa mawe uliosimama kwa miongo kadhaa katika jimbo la Georgia, nchini Marekani? Wengi wa walioujua waliuita “Stonehenge ya Marekani,” wakiufananisha na ule mnara wa kale wa mawe uliopo nchini Uingereza. Lakini kwa wengine ulikuwa zaidi ya sanaa, ulikuwa ujumbe wa siri, ajenda ya dunia mpya, na mwongozo wa kizazi kijacho baada ya maangamizi. Mnara huu ulijengwa mwaka 1980 katika eneo la Elbert County. Jambo lililozua u
2 days ago


Tanzania Kwenye Mizani ya Jumuia ya Madola na Aibu ya Kidiplomasia
Rev. Godwin Chilewa Tamko la Commonwealth Ministerial Action Group (CMAG) la tarehe 10 Julai 2026 ni waraka mzito wenye lugha ya tahadhari, ishara za adhabu zinazotunyemelea, na ujumbe wa wazi kwamba Tanzania imeanza kupoteza uaminifu katika misingi ya utawala bora, haki za binadamu, na demokrasia, misingi ambayo ni uti wa mgongo wa Jumuiya ya Madola. Baada ya matukio ya umwagaji damu tarehe 29 Oktoba 2025, tamko hili halipaswi kusomwa kama maneno ya kawaida ya “diplomasia l
4 days ago


Uchambuzi wa Kiitelijensia Kuhusu Maandamano ya 7 Julai 2026
Na. Rev. Godwin Chilewa Matukio ya Julai 7 yanaashiria mabadiliko ya kimsingi katika mienendo ya upinzani wa kijamii nchini Tanzania. Tofauti na maandamano ya jadi, tukio hili limeonyesha kuibuka kwa mkakati mpya wa upinzani usiohitaji uwepo wa watu mitaani kwa wingi bali unaolenga kuparalyze mifumo ya uchumi na utawala. Hii ni hatari kubwa zaidi kwa dola kuliko maandamano ya wazi, kwa sababu ni vigumu kudhibiti, kugundua mapema, na kukabiliana nayo kwa njia za kawaida za kiu
Jul 7


Je, Serikali ya Tanzania Inalea Makundi ya Kigaidi?
Na. Rev. Godwin Chilewa Kauli ya Shekhe Mwaipopo kwamba ana makundi mawili ya vijana, Mbwa Mwitu na Tiger waliopatiwa mafunzo ya kijeshi, na kwamba watatumika kuwaangamiza vijana watakaoandamana tarehe 7 Julai si kauli ya mzaha. Ni kauli nzito, ya kutisha, na yenye harufu kali ya ugaidi. Ikiwa vyombo vya ulinzi na usalama vitakaa kimya na bila kumkamata shekhe huyo na majeshi yake, basi dunia itachukulia ukimya huo kama hatua ya kuhalalisha vurugu, umwagaji damu, na hofu kama
Jul 5


Serikali Inaogopa Maandamano au Mabadiliko?
Na. Godwin Chilewa Je, serikali inaogopa maandamano—au inaogopa mabadiliko yanayobisha hodi? Hili ni swali ambalo kila anayefuatilia siasa na mustakabali wa Tanzania anapaswa kujiuliza. Hata hivyo kabla ya kutoa jibu rahisi ni muhimu kuangalia mambo kadha wa kadha. Kwa mujibu wa takwimu za Benki ya Dunia na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), zaidi ya asilimia 26 ya Watanzania wanaishi chini ya mstari wa umaskini. Vijana ambao ni zaidi ya asilimia 60 ya idadi ya watu wanaendelea
Jul 5


Tanzania: Kutoka Taifa la Maono Hadi Maandamano na Mauaji. Tumefikaje Hapa?
Na. Godwin Chilewa Kwa miongo kadhaa baada ya uhuru, Tanzania ilisimama kama taa ya matumaini barani Afrika. Chini ya uongozi wa Julius Nyerere, taifa lilijijengea heshima kubwa kimataifa kwa misingi ya siasa za ujamaa, mshikamano wa kijamii, na mchango wake katika harakati za ukombozi wa bara la Afrika. Tanzania ilikuwa nchi, wazo, mfano wa maadili, utu, na uongozi wenye dhamira. Leo, taswira hiyo imechakaa. Malalamiko yameongezeka: rushwa imekithiri, pengo kati ya matajiri
Jul 2
bottom of page


